Social Icons

Pages

Tuesday, August 23, 2016

GERALD HANDO AFUNGA NDOA NA MIRIAM KITENGE

Maharusi Gerald Hando na mkewe Miriam Kitenge wakiingia ukumbini.
Mtangazaji maarufu wa Kipindi cha Joto la Asubuhi katika Kituo cha Radio cha Efm, Gerald Hando amefunga ndoa juzi Jumamosi, Agosti 20, 2026 na mpenzi wake, Miriam Kitenge.

Sherehe ya harusi hiyo iliyokuwa ya aina yake ilifanyika katika Ukumbi wa Golden Tulip uliyopo maeneo ya Posta jijini Dar es Salaam ambapo baadhi ya mastaa walihudhuria huku mwanamitindo maarufu, Sheria Ngowi akiwa ndiye mbunifu wa mavazi ya maharusi hao.

Hando ameuaga ukapera na kuanza kufurahia maisha mapya ya ndoa na mkewe Miriam kama walivyofanya mastaa kadhaa hivi karibuni wakiwemo mchekeshaji maarufu, Emmanuel Mgaya ‘Masanja Mkandamizaji’ wa Orijino Komedi na Mbunge wa Kigoma Mjini, Zitto Kabwe.
Bwana Harusi Gerald Hando akiwa na marafiki zake Edward Urio na Sheria Ngowi.

No comments:

Post a Comment

 
 
Blogger Templates